Kuelekea Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri Duniani, tunajivunia kuadhimisha miaka 10 ya mabadiliko ya kimfumo katika usimamizi na uthibiti wa taka nchini Tanzania!

Udhibiti wa taka unaonyesha ukosefu wa usawa wa kijamii katika kanda mbalimbali, ambapo jamii nyingi za kipato cha chini hazina huduma za usimamizi wa taka na hupambana na matokeo ya uchafuzi wa mazingira ambayo ina athari kubwa kwa afya na maisha yao. Vikundi vilivyo katika mazingira hatarishi, kama vile wanawake, vijana, wakusanya taka, na wakazi wa kiasili lazima wajumuishwe katika suluhu za usimamizi wa taka na wapate fursa, kupitia jukumu hilo, kurejesha hadhi yao husika ya kijamii.

Udhibiti wa taka ni moja ya masuala muhimu ya mazingira ya Tanzania. Miji inayokua kwa kasi sana ina uwezo duni wa kukusanya na kuthibiti taka. Hili husababisha kiasi kikubwa cha taka ngumu zisizokusanywa kutupwa katika sehemu mbalimbali katika miji yote. Sekta ya taka ndiyo mchangiaji mkuu wa uzalishaji wa gesi ya ukaa nchini Tanzania huku taka za ozo zikiwa mchangiaji mkuu wa uzalishaji wa methane kutokana na utupaji taka katika dampo la wazi. Utafiti wa “Zero Waste to Zero Emissions” uliongazia jiji la Dar es Salaam (uk. 54) unaonyesha kuwa utekelezaji wa mfumo wa Taka Sifuri unaweza kupunguza uzalishaji wa gasi ya methane kwa 65% na idadi hii inaweza kusambazwa nchi nzima.

Leo tumezindua Makala ya mfumo wa Taka Sifuri hapa Kituo cha kupokea na kuchakata taka Bonyokwa. Kupitia maonyesho haya, tunalenga kueneza ujumbe wa mfumo wa Taka Sifuri, kushirikiana na serikali, jamii, na wadau wa mazingira kuangazia hatua muhimu ambazo tumefikia pamoja tangu 2019.

Akifungua maonyesho haya mgeni rasmi, Mh. Saady Khimji ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi na Huduma za jamii jiji la Dar es salaam alisema, “Nimefurahishwa sana na kazi nzuri ushirika wa waokota taka wanayoifanya hapa Bonyokwa. Mazingira ni masafi sijakutana na vifurushi vya taka pembezoni wala kwenye mitaro wala taka zilizozagaa hovyo. Ningeomba Taasisi ya Nipe Fagio tushirikiane kwa pamoja ili kuupeleka mfumo huu katika kata zote za Ilala.”

Wilyhard Shishikaye, Mratibu wa Mradi wa Sifuri wa Taka Tanzania kutoka taasisi ya Nipe Fagio alisema "Katika miaka mitano (5) ya utekelezaji wa Taka Sifuri, Nipe Fagio imeweza kutekeleza mifumo ya Taka Sifuri mikoa mitatu (3) ambayo ni Dar Es Salaam, Arusha na Zanzibar."

Aliongeza, “Tumesajili chama cha ushirika cha kwanza kuwahi kutokea nchini cha Wakusanya Taka Bonyokwa kilichopo Bonyokwa Dar Es Salaam chenye wanachama zaidi ya 26, hivyo kutengeneza historia kwa vyama rasmi vya wakusanya taka na kuwa daraja kati ya kutambulika rasmi na kazi zao.”

Kuanzia mitaa yenye shughuli nyingi za Dar es Salaam hadi mandhari tulivu ya Arusha na mwambao mahiri wa Zanzibar, Mfumo wa Taka Sifuri umekuwa ukichochea mabadiliko ya mfumo katika usimamizi wa taka. Kupitia mfumo huu tumefikia kiwango cha 95% cha utenganishaji wa taka katika maeneo ya Dar es Salaam na Arusha. Hii ina maana kwamba 95% ya watu wanaoishi katika jamii za kipato cha chini wamekubali kutenganisha taka zao katika makundi yaliyoamuliwa awali kuwezesha viwango vya juu vya kurejesha taka.

John Yusuph Nsyenge, Mwenyekiti wa Wakusanya Taka Bonyokwa alisema, “Tumeweza kurejesha 75-85% ya taka zote zinazozalishwa katika ngazi ya kaya kupitia mboji, uzalishaji wa chakula cha mifugo na urejelezaji. Tumeweza kuthibiti wastani wa tani 39 za taka kwa mwezi katika kila Mtaa tunachohudumia, ambapo tani 30 ni taka ozo.”

Ajira: Ajira zaidi ya 33 katika sekta ya taka kwa jiji la Dar es Salaam ziliongozeka.

Ubunifu: Tumetengeneza “application” ya ukusanyaji wa ada za taka ambayo hutuma kieletroniki uthibitisho wa malipo kwa kaya kupitia ujumbe mfupi (SMS), kuongeza uwazi wa mfumo na kupunguza ulaghai. Tulitoa huduma za udhibiti wa taka kwa jamii ambazo hazikuwa na ufikiaji wa huduma za usimamizi wa taka kwa kutumia chini ya 15% ya makadirio ya bajeti ya usimamizi wa taka kwa manispaa.

Ushirikiano: Kuendeleza ushirikiano, tumeweza kuwaleta pamoja watoa huduma, wakandarasi, warejelezaji na wakusanyaji taka za kibiashara kwa kuunganisha na muundo wa kukusanya taka ambao unaendana na mfumo wa taka sifuri na kuongeza ufanisi wa mfumo.

Ushawishi wa Serikali: Tulipokea ahadi kutoka kwa serikali ya Zanzibar ya kuondoa ushuru na ada za ukusanyaji taka kutoka kwa vyama vya ushirika vya ukusanyaji taka.

Nje ya Mipaka: Kutokana na matokeo chanya ya mfumo wa Taka Sifuri hapa Tanzania, nchi ya jirani Kenya wameweza kuiga Mfano huu kwa kuanza kutekeleza mfumo huu huko Kisumu.

Mtandao wa Taka Sifuri: Tumezindua mafunzo rasmi ya kwanza ya Taka Sifuri yaliyohususha watekelezaji wa mfumo huu kutoka bara la Afrika, tuliopata waombaji zaidi ya 150 kutoka nchi 25 tofauti ulimwenguni.

Mfumo wa Taka Sifuri unaotekelezwa nchini Tanzania ni jitihada za wazi la jinsi mifumo ya kijamii inavyoweza kuigwa kwa mafanikio na kuingizwa katika mazungumzo ya kitaifa, kukuza haki ya kijamii, na kuleta mabadiliko katika utekelezaji katika miji na nchi nyingi za Afrika. Mfumo huu ni kielelezo kamili, chenye manufaa katika uzalishaji wa ajira, kukabiliana na hali ya hewa, kuongeza ufahamu na haki ya kijamii.

Ana Rocha, Mkurugenzi Mtendaji alihitimisha, "Watu wanapopewa uchaguzi mzuri, wanauchukua. Taka Sifuri sio suluhisho tu; ni dhamira ya mustakabali shirikishi kwa Tanzania, jumuiya ya Afrika Mashariki na kwingineko.”

Aliongeza, "Mfumo wa Taka Sifuri unapendekeza mifumo itakayotatua matatizo ya kimazingira kama Uchafuzi wa hali ya hewa, kuruhusu jamii kuelewa mienendo yake na kuchukua hatua stahiki katika kushughulikia matatizo yao. Mfumo huu unaotekelezwa nchini Tanzania ni jitihada za wazi unaoshirikisha jamii wenye mafanikio unavyoweza kuigwa kwa mafanikio na kuingizwa katika mazungumzo ya kitaifa, kukuza haki ya kijamii, na kuleta mabadiliko katika utekelezaji wa usimamizi wa taka katika miji na nchi nyingi za Afrika.











Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete ameelezea kuridhishwa kwake na kasi ya ukuaji pamoja na uimara wa taasisi za fedha hapa nchini huku akizisisitiza taasisi hizo kuendelea kujiendesha kwa weledi zaidi ili ziweze kuongeza tija katika kuchochea ongezeko la uwekezaji na ukuaji wa uchumi wa nchi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo biashara.

Akizungumza kwenye hafla fupi ya futari iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Dkt Kikwete aliitumia benki ya NBC kama mfano muhimu katika kuthibitisha uimara wa taasisi hizo ambazo pamoja na kuongeza viwango vya mikopo na huduma mbalimbali kwa wateja pia zimeweza kutengeneza faida kubwa na hivyo kuendelea kijiimarisha zaidi.

“Napotoa pongezi na shukrani naamanisha kwa dhati kabisa kwasababu mabadiliko (reforms) mengi ya taasisi ya kifedha yalifanyika mimi nikiwa Waziri wa Fedha kwa wakati ule hivyo najua vema tulipo sasa na tulipotoka. Leo hii nikiona mabenki yanatangaza faida kwa mabilioni ya fedha yananithibitisha wazi kabisa kuwa zile ‘reforms’ tulizozifanya kipindi kile zimefanikiwa,’’ alibainisha Dkt Kikwete huku akiitolea mfano benki ya NBC iliyotengenza faida ya sh bilioni 122 kwa mwaka uliopita.

Akitumia mifano na historia zaidi, Dkt Kikwete alitumia muda mwingi kuelezea namna wateja walivyopitia wakati mgumu kupata huduma za kifedha kwenye taasisi hizo kabla ya serikali kuingilia kati na kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kufunga na kubadili muundo wa uendeshaji na umiliki kwa baadhi ya benki hizo.

‘’Leo hii changamoto zote zimebaki historia. Fedha kwenye Uchumi ndio damu ya Uchumi. Sekta ya fedha ikiteteleka ndio chanzo cha uchumi kuporomoka. Uchumi wa nchi unategemea sekta ya fedha hivyo ikiteteleka kila kitu kinaharibika. Hivyo nawapongeza sana NBC na taasisi nyingine zote kwa kuendelea kutoa huduma zenu kwa weledi huku pia mkiendelea kujiimarisha kimitaji,’’ aliongeza.

Akizungumzia matukio ya benki hiyo ya kuandaa futari kwa ajili ya wateja wake kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini Dkt Kikwete alisema matukio kama haya yanaongeza imani kwa wateja wa benki hiyo kwa kuwa ni moja ya thibitisho kuwa uhusiano wa benki na mteja haushii kwenye biashara pekee bali pia unagusa imani za wateja.

“Matukio ya futari kama haya yanasababisha wateja wenu tunajisikia vizuri kwa kuwa tunaona kwamba tunahudumiwa na benki ambayo pia inajali maslahi yetu kiimani’’ aliongeza.

Awali akizungumzia hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi, alisema ni muendelezo wa utaratibu wa benki hiyo kwa miaka 15 sasa ikilenga kujumuika na wateja wake kama hatua ya kuonyesha mshikamano na umoja katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Alisema benki hiyo inaheshimu sana Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kutokana na ukweli kwamba, ni kipindi ambacho mwanadamu anajiweka karibu na Muumba wake kupitia mfungo na kufanya maombi.

“Huu ni mwezi ambao pia unatukumbusha kufanya kilicho chema mbele za Mungu wetu. Kwa kuwa NBC siku zote tupo karibu imani za wateja wetu tumeamua kuandaa futari hii ili kujumuika na wenzetu kufanikisha hilo.” Alisema Sabi.

Zaidi Sabi aliangazia huduma maalum ya benki hiyo, "La Riba," iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wenye imani ya kiislamu kwa kuzingatia kanuni za dini hiyo katika masuala yanayohusiana na fedha na mtazamo wa dini hiyo kuhusiana na riba.

‘’NBC ndio benki ya kwanza kubwa kuanzisha huduma za kibenki zinazozfuata misingi ya kisheria kupitia La Riba Banking ikiwemo akaunti za akiba na biashara kwa watu binafsi, wajasiriamali na makampuni makubwa. Benki pia inayo akaunti ya muda maalum (fixed deposit) inayofuata misingi ya sharia yaani ‘Mudharaba’. Zaidi kupitia dirisha hilo la La Riba tunatoa huduma ya mikopo kwa wafanyanyabiashara wakubwa na wa kati, wajasiriamali wadogo na wafanyakazi wa sekta ya umma na sekta binafsi,’’ alibainisha Sabi.

Hafla hiyo ya futari ilihudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini wakiongozwa na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Sheikh Walid Alhad Omar, viongozi wa vyama vya siasa, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.



Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete (kushoto) akipokea zawadi maalum kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi (Kulia) wakati wa hafla futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wa jijini Dar es Salaam jana. Hafla hiyo ilifanyika jana jijini humo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.



Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo ilifanyika jana jijini humo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.



Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi (kulia) akimkaribisha Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo ilifanyika jana jijini humo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.


Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Sheikh Walid Alhad Omar (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa ajili ya wateja wake jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo ilifanyika jana jijini humo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.



Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi (pichani) akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo ilifanyika jana jijini humo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.



Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla hiyo.



Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa benki ya NBC pamoja na wateja wa benki hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini humo . Hafla hiyo ilifanyika jana jijini humo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.

Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NBC wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake jijini humo. Hafla hiyo ilifanyika jana jijini humo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wateja, mawakala pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo.
Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) limefanikisha kufungwa kwa mtambo unaoondoa ganda laini la korosho ili kuongeza thamani zao hilo kabla ya kusafirishwa.

Akizungumza leo Machi 29,2024 wakati wa kusaini makubaliano na makabidhiano ya mtambo huo kwa Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (Camartec), Mkurugenzi Mkuu wa Tirdo, Profesa Mkumbukwa Mtambo, amesema lengo ni kuongeza thamani zao hilo kabla ya kusafirishwa.

Amesema walipewa jukumu la kuleta mitambo itakayoondoa ganda laini la korosho kukamilisha mnyororo mzima wa ubanguaji korosho.

Taasisi zingine zilizofanikisha kufungwa kwa mtambo huo ni Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (Temdo) na Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (Sido). 

"Tunaishukuru serikali kwa kuziwezesha taasisi zetu kifedha na kuweza kupata mitambo kama hii," amesema Profesa Mtambo.

Kwa upande wake Mhandisi Atupele Kilindu kutoka Idara ya Uhandisi Maendeleo Tirdo, amesema mtambo huo uliogharimu Sh milioni 40 una uwezo wa kuondoa ganda laini kilo 350 kwa saa.

Amesema lengo ni kuanzisha kiwanda cha mfano kwa ajili ya kufundisha wajasiriamali namna ya ubanguaji na kuongeza mnyororo wa thamani katika zao la korosho.

Kaimu Mkurugenzi wa Camartec, Mhandisi Paythias Ntella, amesema tayari wana kiwanda darasa cha kubangua korosho kilichoanzishwa na kituo hicho wilayani Manyoni mkoani Singida.

Amesema kiwanda hicho kimeanzishwa kwa lengo la kuwasaidia wakulima kubangua korosho na kuacha kuuza zikiwa ghafi na kushindwa kunufaika na kilimo hicho.

"Tunafundisha wajasiriamali katika hatua zote ili kubangua na kumenya ili vitengenezwe viwanda vingi zaidi sehemu nyingine," amesema Ntella.

Lengo la Serikali kuhakikisha asilimia 60 ya korosho zote zinazozalishwa nchini zinabanguliwa ifikapo msimu wa mwaka 2025/26 na asilimia 100 ifikapo mwaka 2030.











KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika Iftar iliyoandaliwa na Kampuni hiyo huku ikitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuendelea kuwaunga mkono sambamba na kuhimiza kudumisha amani.

Hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Kampuni hiyo ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Fatma Abdallah imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa taasisi za umma na binafsi pamoja na wateja wa kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Mgeni rasmi katika Iftar hiyo alikuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Walid aliyewakilishwa na Sheikh wa Wilaya ya Temeke ...

Akizungumza wakati wa Iftar hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni hiyo Dk Selemani Majige ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa ni vema kila Mtanzania kwa nafasi yake kuendelea kuliombea Taifa sambamba na kumuunga mkono Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.

"Tunafahamu kwa sasa tunaendelea na Mfungo wa Ramadhan pamoja na Kwaresima hivyo wakati tukiendelea na Mfungo ni vema tukaliombea Taifa letu lakini wakati huo huo kudumisha Umoja,amani na mshikamano,"amesema Dk Majige.

Amesisitiza kuendelea kudumisha amani katika nchini Kunafanya uchumi Wetu kuendelea kuimarika na biashara zetu ziendelee vizuri."Kulinda amani ni jambo kubwa kwani kama hakuna amani basi hata biashara haziwezi kufanyika vizuri.

"Hivyo kupitia mwezi mtukufu wa Ramadhan ni vema kuendelea kumuomba Mungu na kuendelea kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili aendelee kutuongoza na kudumisha amani katika taifa letu."

Pia amewaomba Watanzania kuendelea kutumia mafuta ya Puma Energy Tanzania pamoja na bidhaa zake zote huku akifafanua mafuta ya Kampuni hiyo yana ubora na viwango vya hali ya juu.

"Tunawaomba muendelee kutumia mafuta ya Puma ili tuongeze faida na tukiongeza faida Serikali inapata gawio na inapotoa gawio zinapatikana fedha ambazo zinakwenda kuhudumia jamii katika maeneo mbalimbali,"

Kwa upande wake Sheikh wa Wilaya ya Temeke Sheikh Zailai Hassan Mkoyogole aliyemwakilishwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Omar aliyekuwa mgeni rasmi, amesema kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan jambo kubwa ni kuzidisha wema kwa maana wanadamu ni wakosaji mbele za Mwenyezi Mungu.

"Binadamu anamkosea Mwenyezi Mungu kwa vitu vingi hivyo sasa ameleta Mwezi mtukufu wa Ramadhan ili kutubu kwa yale yote ambayo ameyafanya.Hivyo kinachotakiwa katika mwezi huu ni kufanya yale yaliyomema na kurejea kwake,"

Pia amesema Mwenye Mungu anapenda kuombwa ,hivyo ametoa mwito kwa watu wote kurejea kwa Muumba kuomba msamaha.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah amewashukuru wadau waliojitokeza katika futari hiyo huku akitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuwaunga mkono kwa kununua bidhaa za mafuta ya Kampuni hiyo.

Aidha amesema wao kama Puma Energy Tanzania wataendelea kuunga mkono juhudi za Serikali hasa katika kutekeleza matumizi ya nishati safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa lengo la kuendelea kutunza mazingira .

"Puma Energy Tanzania tunatambua mwelekeo wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na hasa kwenye suala la nishati safi hivyo tutaendelea kuaidia kwa lengo la kuhakikisha mazingira yanalindwa na matumizi ya nishati safi kwa watanzania yanakuwa kipaumbele."

Wakati huo huo Mkurugenzi Mkuu UDA- RT Waziri Kindamba aliyeshiriki futari hiyo amewapongeza kwa kuandaa futari hiyo ni kuwaalika wateja wao ambao wanatumia vilainishi na mafuta.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania Dk . Selemani Majige akisalimiana na Mkurugenzi wa UDA-RT Waziri Kindamba pamoja na wageni wengine waalikwa waliohudhuria futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah akisalimiana na wageni waalikwa wakati wa hafla ya Iftar iliyofanyikaa jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi Mkuu wa Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah akizungumza na wageni waalikwa wakati wa hafla ya Iftar iliyofanyikaa jijini Dar es Salaam












Na Mwandishi wetu- Dodoma

Serikali kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu inaendelea kuratibu utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na Madhara ya El Nino kuanzia Septemba 2023 hadi Juni 2024.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa-Ofisi ya Waziri Mkuu (SBU) Brigedia Hosea Ndagala katika Kikao Kazi cha kujadili utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na Madhara ya El Nino Septemba 2023 hadi Juni 2024 ambapo alisema kutokea kwa maafa husababisha madhara ambayo huathiri utendaji kazi, kuzorotesha maendeleo na ukuaji wa kiuchumi kwa wananchi na kupotea kwa mafanikio yaliyopatikana kwa muda mrefu na hivyo, kuzorotesha hatua za maendeleo.

Alisema Maafa hayo yamekuwa yakisabibisha madhara mbalimbali ikiwemo vifo, ulemavu wa kudumu, upotevu na uharibifu wa mali na miundombinu, na ongezeko la tegemezi kutokana na Watoto kupoteza wazazi.

“Nchi yetu imekuwa ikishuhudia matukio ya majanga ambayo yamekuwa yakisababisha maafa na kuathiri mfumo wa kawaida wa maisha ya jamii. Maafa haya yamekuwa yakisabibisha madhara mbalimbali ikiwemo vifo, ulemavu wa kudumu, upotevu na uharibifu wa mali na miundombinu,”Alisema Brigedia huyo.

Aidha Brigedia Ndagala alizitaka kila sekta kuwasilisha tathmini ya utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na Madhara ya El Nino ambao una lengo la kuhakikisha serikali na wadau wanachukua hatua stahiki kuzuia au kupunguza madhara na kujiandaa kukabili na kurejesha hali kutokana na maafa yanayosababishwa na El Nino ili kuokoa maisha na mali.

“Hatua hii ni muhimu ili kuweka mikakati ya pamoja kwa ajili ya maandalizi ya msimu wa mvua za Masika. Ni imani yangu kuwa kikao kazi hiki kitatoka na mikakati madhubuti itakayosaidia kuendelea kuongeza ufanisi katika kukabiliana na maafa,” Alieleza.
 

Mkurugenzi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Brigedi Hosea Ndagala akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi Cha Kujadili Utekelezaji Wa Mpango Wa Taifa Wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na madhara ya mvua za El Nino kikao kilichofanyika Jijini Dodoma.
 

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Luteni Kanali Selestine Masalamado akichangia wakati wa wasilisho la Madhara yaliyotokana na mvua za El-Nino katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma.
 

Mkurugenzi wa Udhibiti na Usimamizi wa Ubora wa huduma za hali ya hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Bw. Geofrid Chikojo akitoa wasilisho kuhusu taarifa ya muelekeo wa mvua za msimu wa masika kwa mwezi Machi hadi Mei 2024 katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma.
 

Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Mkoa wa Morogoro Ndug. Anza-Amen Ndossa akichangia mada wakati wa wasilisho lililohusu madhara yaliyotokana na mvua za El-Nino katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma .
 

Picha ya pamoja ya washiriki wa kikao kazi cha Kujadili Utekelezaji Wa Mpango Wa Taifa Wa Dharura wa Kuzuia na Kukabiliana na madhara ya mvua za El Nino katika kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma.


Top News